Thursday, January 19, 2012

KERORO RUKSA BRAZIL 2014.

KATIBU Mkuu wa Shrikisho la Soka Duniani-FIFA Jerome Valcke amesema bia zitauzwa katika viwanja vyote 12 vitakavyotumiwa katika michuano nya Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka 2014. Kauli ya Valcke imekuja kufuatia mvutano wa FIFA na serikali ya nchi hiyo ambayo ilikataza uuzwaji wa vileo katika viwanja vya mpira nchini humo lakini katibu huyo alisisitiza bia lazima zitakuwepo. Upigaji kura kwa ajili kupitisha sheria za Kombe la Dunia ulisimama kufuatia kutofautiana kati ya FIFA na waandaji wa michuano hiyo kuhusu suala la kuuza vileo uwanjani. Akihojiwa kuhusu suala hilo Valcke amesema vileo vimekuwa sehemu ya Kombe la Dunia na hatutahitaji majadiliano kuhusu hilo kwani vileo lazima vitakuwepo katika michuano hiyo. Uuzwaji wa vileo ulipigwa marufuku katika viwanja vyote nchini Brazil mwaka 2003 na imekuwa kama katiba kwa mashabiki ili kuzuia vurugu kwa mashabiki watukutu.

No comments:

Post a Comment