Monday, January 30, 2012

MENSAH KUREJEA UWANJANI KARIBUNI.

NAHODHA wa timu ya taifa ya Ghana John Mensah amesema anaendelea vyema kuvuatia majeruhi ya msuli aliyoyapata katika mchezo wa makundi wa Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi Botswana. Mensah amesema kuwa anajisikia vyema kila siku ambapo daktari wake amesema baada ya kumfanyia uchunguzi jijini Libreville kuwa hayakuwa majeraha makubwa na atarejea uwanjani katika kipindi cha karibuni. Beki huyo tegemeo wa timu hiyo alitolewa nje katika mchezo wa ufunguzi wa kundi D dhidi ya Btswana jijini Franceville lakini alipewa adhabu ya kufungiwa mchezo mmoja hivyo inamaanisha kama akipona sawasawa anaweza kucheza katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi Jumatano. Kurejea kwa Mensah kutampa wakati mgumu kocha wa timu hiyo Goran Stevanovic haswa ikizingatiwa kuwa mabeki wake wote wanne watakuwepo akiwemo Isaac Vorsah ambaye alikuwa akitumikia adhabu ya kufungiwa michezo miwili na John Boye.

No comments:

Post a Comment