Wednesday, January 18, 2012

TEVEZ KUSAINI PSG.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Argentina Carlos Tevez anatarajiwa kusaini mkataba na timu ya Paris Saint German-PSG baada ya klabu hiyo na klabu ya Manchester City kufikia makubaliano. PSG inataka kumsajili mchezaji huyo ambaye hajacheza katika kikosi cha City toka alivyokataa kupasha misuli moto katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mkataba wa miaka mitatu na nusu ingawa ada ya uhamisho haikutajwa. Mabingwa wa Italia klabu ya AC Milan ilishindwa kumnyakuwa Tevez kufuatia mshambuliaji wake kutoka Brazil Alexandre Pato kukataa kujiunga na klabu ya PSG kwa ada ya euro milioni 28.
Mkurugenzi wa Michezo wa PSG Leonardo amekuwa na mawasiliano ya karibu na mchezaji huyo wa ambaye pia ameshawahi kuzichezea klabu za Lazio, Manchester United na Boca Juniors toka mzozo na klabu yake ya City ulipoanza.

No comments:

Post a Comment