Monday, February 27, 2012

DONOVAN KUKOSA MCHEZO WA ITALIA.

MSHAMBULIAJI wa timu ya taifa ya Marekani Landon Donovan atakosa mchezo wa timu yake hiyo dhidi ya Italia baada ya kujiondoa kutokana na maradhi yanayomsumbua. Donovan atakosa nafasi ya kucheza pamoja na Clint Dempsey kwa mara ya kwanza toka kocha Jurgen Klinsmann achukue mikoba ya kuinoa timu hiyo msimu uliopita. Mbali na Donovan mchezaji mwingine wa kikosi hicho ambaye atakosa mchezo huo utakaopigwa jijini Genoa, Italia ni Jermaine Jones ambapo ameumia kifundo cha mguu. Katika kuziba nafasi za wachezaji hao Klinsmann amewaita wachezaji Sasha Kljestan na Brek Shea ambao wanatoka katika kikosi timu ya vijana ya chini ya umri wa miaka 23 ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment