Monday, February 27, 2012

WACHEZAJI WA BRAZIL WASHUTUMIWA KWA UNUNUZI WA NAGARI HARAMU.

Emerson
WAENDESHA Mshtaka nchini Brazil wanawatuhumu wachezaji wa Brazil Emerson na Diguinho kwa kuhusika na shughuli za magendo za kuingiza gari aina ya BMW nchini humo kutoka Marekani kinyume cha sheria. Waendesha mashtaka hao kutoka jiji la Rio de Janeiro wanataka kuwashitaki wachezaji hao kwa magendo pamoja na kutumia fedha chafu na majina yao yalionekana wakati wa uchunguzi wa tukio hilo kuhusu genge hilo ambalo huleta magari kutoka nje na kuuza nchini humo kinyume cha sheria. Kama wachezaji hao watakutwa na makosa hayo waatakabiliwa na kifungo cha miaka 14 jela ambapo hakimu anayesimamia kesi hiyo atapitia vilelezo kabla kuangalia uwezekano wa kuwafungulia mashtaka. Emerson ambaye ni mshambuliaji wa klabu ya Corinthians na Diguinho ambaye ni kiungo wa klabu ya Fluminense zote za nchini humo wamekana makosa hayo wakidai kuwa walinunua magaro hayo kwa kufuata taratibu zote za kisheria.

No comments:

Post a Comment