Wednesday, February 22, 2012

KESHI AMUACHA MIKEL OBI.

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Nigeria Stephen Keshi ameamua kumuacha kiungo wa Chelsea John Mikel Obi katika kikosi cha timu hiyo kitakachocheza na tmu ya taifa ya Rwanda kutokana na majeruhi. Nigeria marufu kama Super Eagles inatarajia kucheza na Rwanda katika Uwanja wa Amavubi uliyopo Mjini Kigali February 29 kwa ajili ya kusaka nafasi ya kucheza fainali za Mataifa ya Mataifa mwaka 2013. Mikel amekuwa nje ya Uwanja katika Klabu yake baada ya kupata majeraha katika mchezo was re ya 1-1 dhidi ya Tottenham Hotspur Diemba mwaka jana huku Keshi akiamua kumuacha katika kikosi chake kwa ajili ya mchezo huo. Kiungo huyo amekuwa nje ya Uwanja kwa wiki saba kutokana na maumivu ya msuli na kuikosa michezo tisa lakini anatarajia kuanza katika kikosi cha kwanza katika mchezo wa FA dhidi ya Birmingham City utakaochezwa katika Uwanja wa Stamford Bridge Jumamosi. Keshi mwenye umri wa miaka 50 amesema yeye ni kama kwa Baba kwa Nyota huyo wa Chelsea mwenye umri wa miaka 24 hivyo hawezi kuhatarisha maisha yake . Wiki iliyopita Keshi aliwaita wachezaji 11 wanaocheza ndani ya nchi hiyo na kuwaacha wachezaji wenye majina makubwa akiwemo Kalu Uche, Brown Ideye, Chinedu Obasi na Mikel.

No comments:

Post a Comment