Monday, February 13, 2012

"MANCINI TREAT ME LIKE A DOG", TEVEZ.

MSHAMBULIAJI wa Manchester City Carlos Tevez amerejea Uingereza akimtuhumu kocha wake Roberto Mancini kwa kumchukulia kama mbwa katika tukio lililopelekea kuondolewa katika kikosi cha timu hiyo ambao ni vinara wa Ligi Kuu nchini humo. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina amesema kuwa Mancini aliapa mbele yake wakati wa mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich ambao walipoteza Septemba mwaka jana ambapo mchezaji huyo alikataa kupasha misuli moto. Tevez hajaichezea City toka September 27 mwaka jana nchini Ujerumani lakini yuko tayari kurejea katika kikosi hicho baada ya kukaa nje ya uwanja kwa muda zaidi ya miezi mitatu. Mancini ameshaonyesha nia ya kumsamehe mchezaji huyo kama ataomba msamaha kwa kosa alilofanya na Tevez wakati akihojiwa na luninga moja nchini Uingereza amesema hadhani kama ana kosa lolote lakini kama klabu inafikiri hivyo anaomba msamaha.

No comments:

Post a Comment