Monday, February 27, 2012

RONALDO ASIFIA BAO LAKE LA KISIGINO.

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amesema bao lake la ushindi dhidi ya Rayo Vallecano aliloshinda kwa kisigino Jumapili kuwa ni la kukumbukwa lakini mchezaji huyo alikataa kulielezea bao hilo kama ni bora zaidi kufunga katika kipindi alichocheza soka. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno ameshafunga mabao 29 baada ya timu yake kuibuka kidedea kwa kushinda bao 1-0 dhidi ya majirani zao hao wanaotoka katika jiji la Madrid. Ronaldo alishinda bao hilo akiwa umbali wa mita 15 kutoka golini ambapo aliugonga mpira kwa kisigino na kuwapita mabeki wapatao wanne na kutinga wavuni. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Ronaldo amesema kuwa siku zote ni tofauti ukishinda bao la kisigino kwa kuwa linakuwa bao zuri lakini hadhani kuwa ndio bao bora toka aanze kusakata kabumbu.

No comments:

Post a Comment