Monday, February 13, 2012

WOLVES YAMTIMUA KOCHA WAKE.

KLABU ya Wolverhampton Wanderers ya Uingereza imemtimua meneja wake Mick McCarthy kutokana na timu hiyo kusuasua kubakia katika Ligi Kuu nchini humo. Mchezo wa mwisho wa kikosi hicho chini McCarthy ulikuwa ni mchezo wa Jumapili dhidi ya mahasimu wao West Bromwich Albion ambapo walipoteza mchezo huo kwa kufungwa mabao 5-1 na kuifanya timu hiyo kutupwa katika mstari wa kusguka daraja. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo Jumatatu ilisema kwamba klabu hiyo imechukua uamuzi huo kutokana na matokeo mwenendo mbovu wa timu hiyo ambapo katika michezo 22 ya ligi iliyocheza imefanikiwa kupata alama 14 tu. Kocha Msaidizi wa Wolves Terry Connor ndiye atayrchukua majukumu ya kukinoa kikosi hicho wakati wakitafuta kocha mwingine atakayeziba nafasi ya MacCarthy.

No comments:

Post a Comment