Tuesday, March 27, 2012

ABIDAL KUPIGWA KISU.

BEKI wa Barcelona, Eric Abidal anatarajiwa kufanyiawa upasuaji wa kupandikiza ini katika hospitali moja nchini Barcelona. Taarifa zilizotolea na klabu hiy zinasema kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa amechangiwa ini hilo atalopandikizwa kutoka kwa rafiki yake wa karibu ambaye wamekuwa wote toka utotoni. Kulikuwa kuna wasiwasi kwamba Abidal asingecheza tena soka ya ushindani baada ya upasuaji kama huo mwaka jana, lakini Mfaransa huyo alipona na kurudi kazini akicheza soka safi katika ushindi wa 3-1 wa Barca dhidi ya Manchester United katika fainali ya Ligi ya Mabingwa kwenye Uwanja wa Wembley. Abidal pia hivi karibuni alisaini mkataba mpya na Barcelona ambao haujaweka wazi ni kwa muda gani mchezaji huyo ataitumikia klabu hiyo..

No comments:

Post a Comment