Tuesday, March 27, 2012

BECKHAM KUUZA MAGARI YAKE YA KIFAHARI.

Moja ya magari ya kifahari ya David Beckham.
HIVI ni kweli Beckham atakuwa ameishiwa? Hapana, inaweza isiwe hivyo. Lakini hilo linaweza kufafanua ni kwanini ameripotiwa kuuza magari yake matano ya kifahari aliyonayo. Gazeti moja la udaku nchini Uingereza la The Sun limeripoti kuwa David Beckham mwenye umri wa miaka 36 ameamua kuuza magari yake ya kifahari ambayo ni mawili aina ya Bentleys, BMW 645, Range Rover Sport pamoja na lingine aina ya Lamborghini Gallardo ambayo yamepaki katika jumba lake la kifahari la Sawbridgeworth. Gari la Lamborghini peke yake lina thamani ya paundi 170,000 au kwa lugha nyingine unaweza kusema mshahara wa siku 10 wa mchezaji huyo. 
Hivi karibuni Beckham alionekana katika jiji la Los Angeles akitumia pikipiki katika matembezi yake maeneo mbalimbali ya mji huo.

No comments:

Post a Comment