Thursday, March 22, 2012

HALI YA HAVELANGE BADO TETE.

Former FIFA President and former IOC member Joai Havelange.
RAIS wa zamani wa Shirikisho la Soka Dunia-FIFA na Mjumbe wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki-IOC Joai Havelange bado anaendelea kupata matibabu akitibu maambukizi aliyopata kwenye kidonda alichopata katika kifundo cha mguu wake wa kulia. Taarifa iliyotoka katika Hospitali ya Samaritano iliyopo katika jiji la Rio de Janeiro imesema kuwa Havelange ambaye ana umri wa miaka 95 hali yake bado si nzuri taarifa ambayo ilipingana na ile iliyotolewa na Shrikisho la Soka nchini humo iliyosema kwamba Havelange anaendelea vizuri. Havelange amewahi kuliongoza shirikisho la soka la Brazil kwa karibu miongo miwili ikiwemo miaka ambayo nchi hiyo ilifanikiwa kunyakuwa Kombe la Dunia mara tatu katika miaka ya 1958, 1962, na 1970. Havelange amekalia kiti cha urais cha FIFA kuanzia mwaka 1974 mpaka 1998 na kubakia kuwa rais wa heshima wa shirikisho hilo ambapo yeye ndio rais wa mwisho kabla ya rais wa sasa Sepp Blatter kushika madaraka hayo.

No comments:

Post a Comment