Friday, March 16, 2012

VURUGU ZAJERUHI 11 COLOMBIA.

POLISI imesema inashikilia watu 135 baada ya vurugu zilizosababisha watu 11 kujeruhiwa nchini Colombia. Mamlaka imesema leo kwamba watu watatu walikuwa wana hali mbaya sana baada ya mashabiki wa Amerika na Deportivo Cali kugombana kabla na wakati wa mchezo katika vurugu zilizoendelea hata baada ya mechi hiyo ya Copa Colombia jana mjini Cali. Mashabiki hao walizipiga licha ya kwamba pande zote mbili za mashabiki wa timu hiyo zilikubaliana amani kuelekea kwenye mchezo huo. Maofisa walisema askari Polisi mmoja alipoteza kidole chake katika mapambano hayo. Jumapili iliyopita, mtu alipigwa risasi na kufariki na wengine tisa walijeruhiwa kwa visu, baada ya mashabiki wa wapinzani wa jadi wa Medellin, Atletico Nacional na Independiente kupigana. Polisi ilisema watu 315 walikamatwa na kukamata visu zaidi ya 450 wakati huo

No comments:

Post a Comment