Monday, April 2, 2012

IRAQ KUIANGUKIA FIFA.

SHIRIKISHO la Soka la Iraq-IFA limelitaka Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuwafungulia ili waweze kucheza michezo ya kirafiki ya kimataifa katika uwanja wao wa nyumbani. Makamu wa rais wa IFA Abdel Khaleq Massoud amesema kuwa watajaribu kuishawishi FIFA kwa kuwapelekea ushahidi kwamba nchi hiyo iko salama kuandaa michezo ya kirafiki. Massoud amesema kuwa rais wa IFA Najeh Hmoud anatajiwa kuongoza jopo la viongozi watakaokwenda kuonana na rais wa FIFA Sepp Blatter jijini Zurich April 13 mwaka huu kuongelea mustakabali wa soka la nchi hiyo. Aliongeza kuwa jopo hilo litajaribu kuiomba FIFA kuwafungulia ili waweze japo kuandaa michezo ya kimataifa ya kirafiki ya timu ya taifa ya nchi hiyo katika uwanja wa nyumbani wakati wakiendelea kuwafungia kucheza michezo ya mashindano nyumbani. FIFA iliifungia Iraq kuandaa michezo katika viwanja vyake vya nyumbani kufuatia vurugu zilizotokea Septemba 2 mwaka jana katika mji wa Kurdistan.

No comments:

Post a Comment