Wednesday, July 11, 2012

SUDAN KUSINI YACHEZA MCHEZO WAKE WA KWANZA WA KIMATAIFA KAMA TAIFA HURU.

Baadhi ya wachezaji wa kikosi cha Sudan Kusini wakijifua.
SIKU baada ya Sudan ya Kusini kusheherekea mwaka mmoja toka wapate uhuru, timu ya taifa ya nchi hiyo ilicheza mchezo wake wa kwanza wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Uganda na kutoka sare ya bao 2-2. Maelfu ya mashabiki wa soka wa nchi hiyo waliojitokeza kushuhudia mchezo huo wa kwanza kwa timu hiyo uliochezwa jana walifurahia kuona timu yao ikitoa sare ya kwanza toka wawe taifa huru Julai 9 mwaka 2011 kwa kuamini kuwa ni mwanzo mzuri wa timu hiyo kuelekea katika mafanikio. Mwanamuziki Margaret Igali ambaye alikongoza kwaya iliyoimba wimbo wa taifa wa nchi hiyo amesema kuwa amefurahi kwasababu hatimaye wamekuwa taifa huru na wana timu yao ya taifa hivyo wanapaswa kujivuani hilo. Naye kocha wa timu hiyo Zoran Dordevic ambaye ni raia wa Serbia amesema kuwa ilikuwa ni kazi kubwa kuandaa wachezaji kucheza na timu ngumu kwa upande wa Afrika Mashariki kama Uganda. Kocha huyo aliendelea kusema kuwa Uganda wamecheza michezo mingi ya kimataifa wakiwa pamoja wakati wachezaji wake bado walikuwa hawajakaa pamoja kwa muda mrefu. Sudan ya Kusini ilijetenga na Sudan na kutangazwa taifa huru Julai 9 mwaka 2011 baada ya miongo mitano ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vimesababisha vifo vya zaidi ya watu milioni mbili na wengine wengi wakiyakimbia makazi yao kwa kwenda maporini na wengine nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment