Sunday, September 23, 2012

ABU TRIKA HAUZWI - AL AHLY.

KLABU kongwe ya soka nchini Misri Al Ahly imetangaza kuwa mshambuliaji wake nyota Mohammed Abu Trika hauzwi na kupinga madai kuwa amepanga kuihama timu hiyo. Mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Haji Khashaba amesema kuwa Trika hajapewa mkataba wowote wa kumfanya kuondoka klabuni hapo. Kauli hiyo imekuja kufuatia tetesi katika magazeti nchini humo kuwa klabu ya Al Nasr ilikuwa katika harakati za kutaka kumnasa nyota huyo katika kipindi cha usajili cha dirisha dogo Januari mwakani. Lakini Khashba alikanusha taarifa hizo na kusema kuwa hawajazungumza lolote na Al Nasr kuhusiana na suala la uhamisho la mchezaji huyo na hawana mpango wa kumuuza kwa bado wanamuhitaji. Trika anatarajiwa kucheza katika mchezo wa kirafiki kati ya Ahly na Sunshine Stars pamoja na maamuzi ya bodi ya klabu hiyo kumfungia miezi miwili baada ya kukataa kucheza katika mchezo wa Super Cup ingawa baadae aliomba radhi kutokana na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment