Sunday, September 23, 2012

HENRY KUUKARABATI UWANJA WA ANFIELD.

MMILIKI wa klabu ya Liverpool kutoka Marekani John Henry anatarajiwa kumaliza utata wa miaka 10 kwa kujitolea kuendeleza Uwanja wa Anfield ufikie uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 vikiwemo viti vya ziada 7,000.
Hatahivyo kumekuwepo na taarifa kuwa mpaka sasa hakuna makubaliano yoyote yaliyofikiwa kati ya suala la kuufanyia ukarabati uwanja huo au kujenga mwingine mpya katika eneo lingine tofauti na hapo Anfield. Kazi hiyo ya kupanua uwanja huo inatarajiwa kutumia kiasi cha paundi milioni 150 ikiwa ni tofauti kubwa na kujenga uwanja mpya ambao utaigharimu timu hiyo paundi milioni 400 ingawa mpaka sasa paundi milioni 50 tayari zimeshatumika katika miradi na michoro ya uwanja mpya. Halmashauri ya jiji la Liverpool imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na klabu hiyo kuhusiana na suala la uwanja kwa miaka kadhaa ambapo wamekuwa wakitoa nafasi kubwa kujengwe uwanja mpya ambao watautumia pamoja na majirani zao klabu ya Everton. Kwasasa uwanja wa Anfield una uwezo wa kupokea mashabiki 45,000 pekee wakizidiwa na klabu kama Manchester United ambayo uwanja wake wa Old Traford una uwezo wa kubeba mashabiki 76,000 wakati Arsenal uwanja wao wa Emirates una uwezo wa kubeba mashabiki 60,000.

No comments:

Post a Comment