Sunday, September 23, 2012

HAKUNA WA KUZIBA PENGO LA XAVI BARCELONA - FABREGAS.

KIUNGO nyota wa klabu ya Barcelona, Cesc Fabregas amemmwagia sifa mkongwe wa klabu hiyo Xavi Hernandez kwamba amekuwa nguzo muhimu katika kipindi chote ambacho amecheza hapo. Kauli ya Fabregas imekuja kufuatia Barcelona kuhangaika kuipita ngome ya Granada katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Hispania jana usiku kabla ya kiungo huyo mwenye miaka 32 kufanikiwa kufunga bao katika dakika za lala salama na kuipa ushindi wa mabao 2-0. Fabregas ambaye alirejea katika klabu yake hiyo baada ya kuondoka kwenda Arsenal mwaka 2006 anaamini kuwa pengo la Xavi litakuwa gumu kuzibika wakati wake wa kustaafu utapofika. Barcelona imeendeleza rekodi yake nzuri ya kushinda michezo yake yote mitano ya ligi waliyocheza msimu huu na kuwaacha mbali mahasimu wao ambao ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo Real Madrid baada ya kuanza msimu wao vibaya kwa kupoteza baadhi ya michezo.

No comments:

Post a Comment