Sunday, September 23, 2012

NTAJIHAMI DHIDI YA MALDONADO - HAMILTON.

DEREVA wa magari yaendayo kasi maarufu kama langalanga kutoka timu ya McLaren, Lewis Hamilton amesema atajitahidi kuwa mwangalifu zaidi katika mashindano ya Singapore Grand Prix ili kuhakikisha hapati ajali. Hamilton anatarajiwa kuanza mbio hizo akiwa sambasamba na Pastor Maldonado wa timu ya Williams ambaye waligongana miezi 18 iliyopita. Akihojiwa Hamilton amesema kuwa katika mbio hizo atajaribu kuwa mwangalifu na kukaa mbali na mpinzani wake huyo na anatarajia na yeye atafanya hivyo. Hamilton na Maldonado waligongana katika mashindano ya Grand Prix ya Ulaya na kupelekea gari la Hamilton kushindwa kuendelea na mashindano hayo huku naye Maldonado akikosa nafasi ya kumaliza katika nafasi za juu.

No comments:

Post a Comment