Sunday, September 23, 2012

BARCELONA YAENDELEZA UBABE HISPANIA.

KLABU ya Barcelona imeendeleza wimbi lake la ushindi katika Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga baada ya kufanikiwa kuifunga Granada kwa mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Camp Nou jana usiku.
Timu hiyo ilibidi ifanye kazi ya ziada baada ya Granada kutaka kugawana alama lakini bao la mchezaji Xavi Hernandez alilofunga dakika tatu kabla ya mpira kumalizika liliihakikishia ushindi wa alama zote tatu timu hiyo. Mara baada ya bao hilo Granada walionekana kushindwa kumudu vishindo vya Barcelona waliokuwa wakishambulia kwa kasi lango la wapinzani wao ambapo kabla ya kipenga cha mwisho beki wa timu hiyo alijifunga mwenyewe akiwa katika harakati za kuokoa shuti la chini kwa chini lililopigwa na mshambuliaji nyota wa timu hiyo Lionel Messi. Ushindi huo umeipaisha Barcelona ambao wanaongoza ligi hiyo wakiwa na alama 15 katika michezo mitano waliyocheza wakiongeza pengo la tofauti ya alama 11 na mahasimu wao Real Madrid ambao watacheza na Rayo Vallecano baadae leo wakisaka ushindi wa kwanza ugenini.

No comments:

Post a Comment