Friday, September 21, 2012

FIFA YAIONYA JAMAICA JUU YA SUALA LA KUVAMIA UWANJA MASHABIKI WAKE.

JAMAICA imeonywa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA juu ya suala la kuvamia uwanja kufuatia ushindi wa kushangaza wa mabao 2-1 wa timu hiyo dhidi ya Marekani katika mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia uliochezwa mwezi huu. Mamia ya mashabiki wenye furaha wa nchi hiyo walikimbia kuvamia uwanja mara baada ya filimbi ya mwisho kupulizwa na kwenda kuwapongeza wachezaji wa timu hiyo baada ya kupata ushindi wake wa kwanza dhidi ya Marekani. Katika taarifa yake ambayo imetimwa kwa Shirikisho la Soka la Jamaica-JFF, FIFA imesema kuwa hilo litakuwani onyo la mwisho kwa nchi hiyo kuzuia tukio kama hilo kutotokea tena. Rais wa JFF, Horace Burrell ameahidi kuwa watakuwa makini kuimalisha ulinzi katika michezo itakayokuja ili kuzuia matukio kama hayo kutokea tena. Guatemala, United States na Jamaica wote wana alama saba kutokana na michezo minne waliyocheza katika kundi A amapo Jamaica inakabiliwa na mchezo mwingine dhidi ya Antigua unaotarajiwa kuchezwa Octoba 16 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment