Friday, September 21, 2012

DROGBA AFURAHIA MAISHA YA CHINA.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba amesisitiza kuwa ana furaha kuwepo nchini China na amepanga kuitumikia miaka miwli na nusu ya mkataba wake katika klabu ya Shanghai Shenhua. Drogba mwenye umri wa miaka 34 aliondoka katika klabu ya Chelsea majira yakiangazi na kujiunga na Shanghai. Kumekuwa na taarifa kuwa matatizo ya kifedha yanayoikabili klabu hiyo yanaweza kumkimbiza mchezaji huyo kurejea katika klabu za Ligi Kuu nchini Uingereza. Drogba ambaye ameshafunga mabao matano katika michezo saba aliyocheza katika timu hiyo amedai kuwa anafurahia kuwepo nchini humo ingawa akakiri kuwa anaipenda ligi ya Uingereza kwakuwa ndio ligi bora duniani lakini hajutii uamuzi wake wa kuondoka. Drogba alifunga mabao 157 katika kipindi cha miaka nane ambayo ameitumikia Chelsea na alikuw nguzo muhimu kuiwezesha klabu kunyakuwa taji lake la kwanza la Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment