Monday, September 24, 2012

HORNE ASHTUSHWA NA TAARIFA ZA TERRY.

Katibu Mkuu wa chama cha soka cha Uingereza- FA- Alex Horne ameelezea kustushwa kwake na maamuzi ya JOHN TERRY ya kustaafu kucheza soka la kimataifa. Terry mwenye umri wa miaka 31 hapo jana alitoa taarifa ya kuachana na soka la kimataifa saa 24 kabla ya FA kusikiliza kesi ya tuhuma za kibaguzi inayomkabili dhidi ya mchezaji wa Queens Park Rangers Anton Ferdnand ambapo amedai chama hicho kimefanya nafasi yake katika timu ya taifa kuwa ngumu. Nahodha huyo wa Chelsea ambaye amewahi kunyang’anywa unahodha wa Uingereza na FA mara mbili amesema kitendo cha chama hicho kuendelea na uchunguzi wa mashtaka dhidi yake wakati Mahakama ikiwa tayari imefanya uamuzi na kumkuta hana hatia inamnyima nafasi ya kutimiza wajibu wake katika timu ya Taifa. Lakini Horne akizungumzia kuhusu kesi hiyo inayotarajia kusilikizwa hii leo katika Uwanja wa Wembley amesema hadhani kama FA imemnyima Terry nafasi katika timu ya taifa na kesi hiyo haihusiani na masuala ya kimataifa ya mlinzi huyo. Kama FA itamkuta Terry na hatia ya kumtolea maneno ya kibaguzi mchezaji huyo Octoba 23 mwaka huu huenda akafungiwa kucheza michezo ya ndani kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment