Friday, September 28, 2012

CHELSEA USO KWA USO NA ARSENAL.

KLABU ya Chelsea inatarajia kuendelea kujikita kileleni mwa Ligi Kuu nchini Uingereza kwa kushinda mchezo wao wa kesho dhidi ya mahasimu wao wa jiji la London Arsenal katika mchezo wao wa kwanza toka nahodha wao John Terry afungiwe kutokana na ubaguzi wa rangi. Terry amefungiwa mechi nne na Chama cha Soka cha Uingereza-FA jana baada ya kukutwa na hatia ya kumfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi beki wa timu ya Queens Park Rangers-QPR Anton Ferdinand na pia kutozwa faini ya paundi 220,000. Terry amepewa siku14 toka atapopokei barua ya uamuzi uliofikiwa na FA kukata rufani kama hakuridhishwa na hukumu hiyo aliyopewa kufuatia tukio hilo ambalo lilitokea wakati wa mchezo wa baina ya Chelsea na QPR uliochezwa katika Uwanja wa Loftus Road Octoba 23 mwaka jana. Adhabu hiyo haitaanza kufanya kazi mpaka muda wa kukata rufani utakapokwisha hiyo inamaanisha kuwa beki huyo atakuwepo katika mchezo wa kesho dhidi ya Arsenal ambao utachezwa katika Uwanja wa Emirates.

No comments:

Post a Comment