Friday, September 28, 2012

XAVI AWABEZA MAHASIMU WAO MADRID.

KIUNGO nyota wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez anafikiri kuwa kuongoza kwao kwa alama nane zaidi ya Real Madrid kunawapa wakati mgumu mahasimu wao hao katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga. Barcelona ambao kiwango chao kimekuwa kinapanda na kushuka msimu huu kutokana na mabeki wake tegemeo kuwa kupata majeruhi ya mara kwa mara watasafiri kuifuata Sevilla kesho ili kutafuta ushindi wake sita ukilingasha na Madrid ambao wameshinda wameshinda mechi mbili pekee msimu huu. Xavi amesema kuwa unapokuwa mbele kwa alama unakuwa unacheza kwa kutulia zaidi kuliko nafasi waliyonayo mahaimu wao Madrid ambao hivi sasa inabidi washinde kila mchezo ili kupunguza pengo. Tatizo kubwa la Barcelona msimu huu limekuwa ni kwa mabeki wake ambapo Gerard Pique Carles Puyol na Adriano wote ni majeruhi lakini kiungo wa zamani wa Arsenal aliyesajiliwa msimu huu Alex Song ameonekana kumudu vyema nafasi ya beki wa kati katika michezo ya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment