Friday, September 28, 2012

KOMBE LA DUNIA 2014 BRAZIL KUCHEZWA MCHANA.

BAADHI ya timu zitakazoshiriki michuano ya Kombe la Dunia 2014 zinatarajiwa kucheza mechi za mchana katika baadhi ya viwanja nchini Brazil baada ya kutolewa ratiba ya muda zitakapochezwa mechi za michuano hiyo. Mechi nyingi kati ya 64 zinatarajiwa kuchezwa mchana kitu ambacho hakitakuwa na tatizo kwa miji iliyopo upande wa Kusini mwa nchi hiyo ambapo kuna baridi lakini inaweza kuwa tatizo kwa wachezaji kucheza katika katika joto kali kwa timu ambazo zitapangwa katika miji iliyopo upande wa Kaskasini na Kaskazini-Mashariki. Jografia ya nchi hiyo inaonyesha kuwa kipindi cha mwezi June na Julai ni kipindi cha baridi kwa miji iliyopo upande wa Kusini mwa nchi hiyo lakini hali huwa ya kitropiki yaani joto katika sehemu za Kaskazini. Sehemu kubwa ya nchi ya Brazil imepishana masaa matatu na bara la Ulaya kitu ambacho kitakuwa kizuri kwa watazamaji wa televisheni wa bara hilo ambao watakuwa wakiona michuano hiyo jioni. Lakini muda huo utakuwa mzigo mkubwa kwa watazamaji wa bara la Asia itabidi wasubiri mpaka usiku wa manane ili waweze kushuhudia michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment