Friday, September 28, 2012

HAMILTON AHAMIA MERCEDES.

Dereva nyota wa mbio za magari yaendayo kasi ya Langalanga, Lewis Hamilton anatarajiwa kuihama timu ya McLaren baada ya kusaini mkataba na timu ya Mercedes kwa ajili ya msimu ujao. Uhamisho huo utamlazimu dereva nyota kutoka Ujerumani Michael Schumacher kuondoka katika timu ya Mercedes lakini bado haijakuwa wazi kama nguli huyo atastaafu au atatafuta timu nyingine kwa ajili ya msimu ujao. Dereva kutoka timu ya Sauber, Sergio Perez ndio amesajiliwa na MacLaren ili kuziba pengo la Hamilton. Uamuzi huo wa Hamilton utakuwa ni pigo kubwa kwa MacLaren ambapo sasa itabidi waendelee bila ya kuwepo kwa dereva wao huyo ambaye wamekuwa nae toka akiwa na umri wa miaka 13.

No comments:

Post a Comment