Thursday, September 27, 2012

WENGER AMSIHI WALCOTT KUWA NA SUBIRA.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amempongeza mshambuliaji wake nyota Theo Walcott kwa kiwango alichokionyesha jana lakini amemwambia kuwa inabidi awe mvumilivu kuhusu ombi lake la kubadilishwa na kuwa mshambuliaji wa kati. Walcott mwenye umri wa miaka 23 alifunga mabao mawili katika ushindi wa mabao sita iliyopata timu hiyo katika mzunguko wa tatu wa michuano ya Kombe la Capital One. Wenger alimsifu mchezaji kwa uwezo wake mkubwa wa kumalizia pindi awapo mbele goli lakini kwasasa amemuomba awe mvumilivu kwakuwa kuna mchuano mkubwa wa kugombea namba ya sehemu hiyo na timu inafanya vizuri. Meneja huyo ambaye kwasasa amuwa akipenda kumtumia mshambuliaji nyota wa kimataifa kutoka Ivory Coast, Gervinho amesema kuwa muda wa Walcott kutumika katika nafasi hiyo utawadia.

No comments:

Post a Comment