Thursday, September 27, 2012

MECHI ZA CAPITAL ONE CUP MZUNGUKO WA NNE.

KLABU ya Chelsea inatarajiwa kupambana na Manchester United katika mzunguko wa nne wa michuano ya Kombe la Ligi baada ya kushinda michezo yao dhidi ya Wolves na Newcastle katika mzunguko wa tatu. Mabingwa watetezi Liverpool ambao walifanikiwa kuifunga West Bromwich wataikaribisha Swansea katika Uwanja wa Anifield mchezo ambao utashuhudia meneja wa timu hiyo Brendan Rodgers akipambana na klabu yake ya zamani. Leeds United ambao walipata ushindi wa kushangaza wa mabao 2-1 dhidi ya Everton Jumanne watakuwa wageni wa Southampton katika Uwanja wa Elland Road, wakati Aston Villa baada ya kuwaondosha mabingwa wa ligi kuu Manchester City wenyewe wataifuata timu ya Swidon katika mzunguko wa nne. Arsenal ambao walitinga fainali ya michuano hiyo mwaka 2011 wataifuata Reading wakati meneja wa Tottenham Hotspurs Andre Villas-Boas atakipeleka kikosi chake kupambana na Norwich. Katika michezo mingine ya mzunguko wanne ya michuano hiyo Wigan itacheza na Bradford wakati Sunderland itaikaribisha Middlesbrough.

No comments:

Post a Comment