Monday, September 24, 2012

SENEGAL YAPANGA KUMFUNGULIA DIOUF.

NAFASI ya mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal El-Hadji Diouf kuitumikia timu yake ya taifa inaonekana bado ipo tofauti na ilivyokuwa mwaka uliopita.
Mshambuliaji huyo anayecheza katika klabu ya Leeds United ambaye alifungiwa miaka mitano kujishughulisha na shughuli zozote za kimichezi nchini kwake anaweza kupumua baada ya Shirikisho la Soka la nchi hiyo-FSF kusema kuwa litaangalia upya adhabu hiyo. Akiohijiwa kuhusiana na suala hilo Makamu wa Rais wa FSF Louis Lamonte alithibisha kuwa ni kweli wamekuwa katika vikao vya kujadili juu ya kupunguza adhabu hiyo ya Diouf katika vikao vyake ambavyo imekaa hivi karibuni. Lamonte amesema kuwa Diouf ameifanyia mengi mazuri nchi yake katika soka ambayo vijana wa nchi nzima wangependa kufikia mafanikio hayo nduio maana wameona ni vyema kuweka suala hilo mezani na kuliangalia upya. Lamonte pia amesema Diouf ni mmoja ya wachezaji wachache ambao walihudhuria katika mechi ambazo timu ya taifa ya nchi hiyo ilicheza jijini Coventry katika michuano ya Olimpiki huku akijitegemea mwenyewe kwa usafiri.

No comments:

Post a Comment