Tuesday, September 18, 2012

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: VIWANJA NANE KUWAKA MOTO ULAYA LEO.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Roberto Mancini ametamba kuwa kikosi chake kimejiandaa vyema kwa ajili ya mchezo wa ufunguzi wa michuano ya Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya Real Madrid katika Uwanja wa Santiago Bernabeu baadae usiku. Mancini alitamba kuwa msimu huu amekiandaa kikosi chake vyema kwa ajili ya kuhakikisha wanafika mbali kwenye michuano hiyo na watadhihirisha hilo wakati watakapokutana na Madrid usiku wa leo. Mbali na mchezo huo pia kutakuwa na michezo mingine ambapo Arsenal watakuwa wageni wa timu ya Montpellier ya Ufaransa, AC Milan itaikaribisha Anderlech, Paris St Germain-PSV itawakaribisha Dynamo Kiev huku mabingwa wa soka wa Ujerumani Borussia Dortmund wataikaribisha Ajax Amsterdam. Michezo mingine Malaga ya Hispania itaikaribisha Zenit St Petersburg ya Urusi, Dinamo Zagreb itakuwa wenyeji wa FC Porto ya Ureno wakati Olympiacos ya Uturuki itawakaribisha Schalke 04 ya Ujerumani.

No comments:

Post a Comment