Tuesday, October 23, 2012

CHIPOLOPOLO KUKWAANA NA BAFANA BAFANA SOCCER CITY.

RAIS wa Chama cha Soka nchini Zambia-FAZ, Kalusha Bwalya amethibitisha kuwa mabingwa wa Afrika watachuana katika mchezo dhidi ya Bafana Bafana katika Uwanja wa Soccer City jijini Johannesburg Novemba 14 mwaka huu. Mchezo baina ya timu hizo umekuwa ukijulikana muda mrefu lakini uwanja ambao ungetumika kwa ajili ya mchezo ndio ulikuwa haujajulikana mpaka Bwalya alipothibisha katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter. Itakuwa ni mara ya tatu kwa Bafana Bafana kuutumia uwanja huo ambao ulijengwa upya kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010 ambapo mara ya kwanza kuutumia uwanja huo waliifunga Colombia mabao 2-1 katika mchezo wa kujipiama nguvu na baadae kutoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mexico katika mchezo wa ufunguzi. Afrika Kusini imecheza na Zambia mara nyingi zaidi toka nchi hiyo iliporuhusiwa kucheza michezo ya kimataifa mwaka 1992 ambapo wamekutana mara 14 huku kila nchi ikishinda michezo minne na kutoa sare michezo sita.

No comments:

Post a Comment