Tuesday, October 23, 2012

GYAN NAHODHA MPYA BLACK STARS.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah ametangaza kuwa Asamoah Gyan ameteuliwa kuwa nahodha mpya wa kikosi hicho maarufu kama Black Stars. Uteuzi huo mpya unafuatia uamuzi wa kumuengua John Mensah katika nafasi hiyo ambayo amekuwa akishikilia kwa kipindi kirefu. Akihojiwa kuhusu uteuzi wake huo Appiah amesema kuwa Mensah ataendelea kuwa mjumbe muhimu katika kikosi chake lakini kwasasa ameamua kufanya mabadiliko kwa ajili ya faida ya nchi hiyo. Appiah aliwaomba wachezaji na wadau wa soka nchini humo kumpa ushirikiano Gyan ili aweze kuingoza Ghana kupata mafanikio katika changamoto zilizoko mbele yao.

No comments:

Post a Comment