Tuesday, October 23, 2012

FEDERER AANZA VYEMA MICHUANO YA SWISS INDOORS.

MCHEZAJI nyota wa tenisi namba moja katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanaume, Roger Federer ameanza vyema kampeni yake ya kutafuta taji la sita la michuano ya ndani ya Switzerland baada ya kumfunga Benjamin Becker kwa 7-5 6-3 na kutinga hatua ya pili ya michuano hiyo. Becker raia wa Ujerumani ambaye anashika nafasi ya 83 katika orodha hizo aliingia katika michuano hyo kuchukua nafasi ya Jeremy Chardy kutoka Ufaransa ambaye aliumia. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Federer amesema kuwa alijiandaa vyema kukabiliana na Becker ambaye mara ya mwisho kucheza naye ilikuwa mwaka 2010 baada ya Chardy kuumia hivyo anashukuru kumfunga mjerumani huyo na kusonga mbele. Federer ameshinda mataji matano kati ya sita ya michuano hiyo ambayo inachezwa katika viwanja vya St Jacobshalle ambako ndiko nyota huyo alipoanzia kucheza tenisi akiwa kama muokota mipira miongo miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment