Thursday, October 25, 2012

IVORY COAST, TOGO, TUNISIA, ALGERIA KUNDI LA KIFO AFCON 2013.

WENYEJI wa michuano ya Mataifa ya Afrika 2013, Afrika Kusini itakata utepe wa michuano hiyo kwa kucheza na Cape Verde ambao waliwashangaza mabingwa wa zamani wa Afrika Cameroon na kukata tiketi ya kushiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza. Morocco ambao watakuwa wenyeji wa michuano hiyo mwaka 2015 sambamba na Angola ndio wanakamilisha timu za kundi A. Mabingwa watetezi wa michuano hiyo Zambia wamepangwa kundi moja na Nigeria pamoja na Ethiopia na Burkina Faso katika kundi C huku kundi B likiwa na timu za Ghana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Niger na Mali. Katika Kundi D ambalo wadau wengi wa mchezo wa soka wanasema ndio kundi la kifo lina timu za Ivory Coast, Togo, Tunisia na Algeria ambapo michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 19 mpaka Februari 10 mwakani.

No comments:

Post a Comment