Monday, November 19, 2012

DJOLIBA, LEOPARDS ZATOKA SARE YA MABAO 2-2 KATIKA FAINALI YA KWANZA YA KOMBE LA SHIRIKISHO.

TIMU ya Djoliba ya Mali imelazimishwa sare ya mabao 2-2 na timu ya AC Leopards ya Congo katika fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho iliyopigwa jijini Bamako jana usiku. Wageni Leopards ndio walikuwa wa kwanza kuona lango la wenyeji wao dakika ya 21 kupitia kwa mchezaji Rochel Fernand kabla ya Alou Bagayoko kuisawazishia Djoliba kwa penati dakika 10 baadae na kunyanyua matuamaini ya mashabiki wengi waliojitkeza kuishangilia timu yao katika Uwanja wa 26 Mars. Kipindi cha pili wenyeji walionyesha juhudi za kutafuta ushindi kwa kushambulia lango la wapinzani kasi na juhudi zao zilizaa matunda dakika ya 73 baada ya beki wa Djoliba kuifungia bao la kuongoza na kuwafanya mashabiki waliojitokeza uwanjani hapo kulipuka kwa furaha. Zikiwa zimebakia dakika tano kabla ya mpira kumalizika Heritier Ngouelou wa Leopards aliwanyamazisha mashabiki waliokuwa wakijua wameshinda mchezo huo kwa kufunga bao la kusawazisha. Matokeo hayo yatakuwa sio mazuri kwa Djoliba ambao wiki ijayo watasafiri kuelekea jijini Dolisie kwa mchezo wa marudiano dhidi ya Leopards, mchezo ambao utaamua bingwa wa Kombe la Shirikisho kwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment