Monday, November 19, 2012

HAMILTON ASHINDA MBIO ZA GRAND PRIX ZA MAREKANI.

DEREVA nyoya wa Langalanga, Lewis Hamilton wa timu ya McLaren amefanikiwa kushinda mbio za Marekani za Grand Prix baada ya kufanikiwa kumpita katika dakika mwisho Sebastian Vettel wa timu ya Red Bull. Katika mashindano hayo Hamilton alionekana kumfukuza kwa karibu Vettel toka mwanzo na baadae kufanikiwa kumpita ikiwa imebakia mizunguko 14. Nafasi ya tatu katika mashindano hayo ilishikwa na Fernando Alonso wa timu ya Ferrari hivyo kufanya mbio za ubingwa mwaka huu kuwa wazi kwa kubakisha alama 13 nyuma ya kinara Vettel. Mashindano ya mwisho yatakayofanyika nchini Brazil mwishoni mwa wiki ijayo ndio yatakayoamua bingwa wa dunia kwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment