Monday, November 19, 2012

NYOTA WA ZAMANI WA UNITED AFARIKI DUNIA.

NYOTA wa zamani wa klabu ya Manchester United ambaye ni mmoja wa wachezaji waliopona katika ajali ya ndege iliyotokea jijini Munich, Ujerumani mwaka 1958, Kenny Morgans amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 73. Katika taarifa iliyotumwa katika tovuti ya United imebainisha kuwa Morgans alikimbizwa hospitali Jumamosi baada ya kuugua ghafla na baadae kufariki dunia katika hospitalini. Nyota huyo ambaye alikuwa winga alianza rasmi kucheza katika kikosi cha kwanza cha United katika mchezo dhidi ya Leicester City Desemba mwaka 1957 akiwa na umri wa miaka 18. Morgans aliumia wakati ndege iliyokuwa imepakia wachezaji wa United wakitokea jijini Belgrade kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Ulaya wakati walipopata ajali hiyo baada ya kujaza mafuta jijini Munich na kuua watu 23 kati ya 44 waliokuwepo katika ndege hiyo. Katika ajali hiyo Morgans alipatikana baadaye joni akiwa amebanwa kwenye viti vya ndege hiyo na waandishi wawili wa Ujerumani na baadae alifanikiwa kupona na kurejea tena uwanjani kabla ya kuhama Old Traford mwaka 1961 kwenda Swansea City.

No comments:

Post a Comment