Saturday, November 17, 2012

RONALDO AKIRI KUM-MISS FERGUSON.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amekiri kuwa amemkumbuka meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson na kumuelezea kuwa kama baba yake katika soka. Ronaldo mwenye umri wa miaka 27 kwasasa anacheza chini ya Jose Mourinho baada ya uhamisho uliovunja rekodi wakati akiondoka Old Traford ambao ulifikia euro milioni 100. Pamoja na kushinda taji la La Liga msimu uliopita na kufunga mabao 46 katika michezo 38 ya ligi hiyo Ronaldo ambaye ni raia wa Ureno aliweka wazi kuwa bado ni mshabiki mkubwa wa Ferguson pamoja na na kuondoka United miaka mitatu iliyopita. Ronaldo alimsifu kocha huyo kwa kumfundisha mambo mengi na kumfanya kuwa mchezaji bora kama alivyosasa hivyo anamuona kama baba yake katika soka ndio hawezi kuacha kumkumbuka Ferguson. Pamoja na umri wa miaka 71 aliokuwa nao Ferguson lakini Ronaldo anaamini kuwa kocha huyo bado ana vitu vingi vya kuisaidia United ili iweze kupata mafanikio zaidi.

No comments:

Post a Comment