Wednesday, November 14, 2012

UNITED NAYO YAINGIA KATIKA MBIO ZA KUMUWANIA ZAHA.

KLABU ya Manchester United inajiandaa ktika mbio mbio za kumnasa kinda wa klabu ya Crystal Palace, Wilfried Zaha. Meneja wa United Sir Alex Ferguson amekuwa akifuatilia maendeleo ya kinda huo kwa miezi kadhaa na sasa ameamua rasmi kusajili katika kipindi cha dirisha dogo la usajili Januari mwaka huu. Mbali na United pia klabu za Arsenal, Liverpool, Manchester City na Tottenham Hotspurs nazo zimekuwa zikimfuatilia winga huyo na wako tayari kuanza mbio za kumsajili katika kipindi cha dirisha dogo la usajili. Mkataba wa Zaha katika klabu hiyo ya ligi daraja la kwanza unaishia 2017 na Mwenyekiti wa klabu hiyo amedai kuwa klabu itakayomhitaji nyota huyo itabidi itoe paundi milioni 20 ingawa dau hilo linaonekana kubwa sana hivyo linaweza kushuka mpaka paundi milioni 10.

No comments:

Post a Comment