Friday, December 28, 2012

ARSENAL YAMTENGEA VILLA PAUNDI MILIONI 16.

KLABU ya Arsenal imetangaza dau la paundi milioni 16 kwa ajili ya kumnasa mshambuliaji wa Barcelona, David Villa. Meneja wa klabu hiyo Arsene Wenger ameonyesha nia ya kumtaka mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 lakini maofisa wa Arsenal wameambiwa kuwa watahitajika kulipa kiasi cha paundi milioni 20 kama watahitaji kumng’oa mshambuliaji hyo wa kimataifa wa Hispania. Hatahivyo kiasi hicho cha fedha kilichotajwa na Barcelona kinaweza kuwa kikubwa kwa Arsenal kwasababu ya umri wa Villa. Mbali na Arsenal Chelsea nao wameonesha nia ya kutaka kumsajili nyota huyo ambaye ni mfungaji wa kihistoria nchini Hispania ili aweze kusaidiana na Eden Hazard na Fernando Torres katika safu ya ushambuliaji wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment