Sunday, December 30, 2012

BOJAN ATAREJEA TENA BARCELONA - BABA

BABA wa mshambuliaji nyota wa zamani wa klabu ya Barcelona Bojan Krkic amesema mwanae huyo anaweza kurejea tena katika klabu hiyo pamoja na kutong’aa katika Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama Serie A. Mshambuliaji huyo aliuzwa kwenda klabu ya AS Roma mwaka 2011 kwa ada ya paundi milioni 12 lakini alitolewa tena kwa mkopo katika klabu ya AC Milan msimu huu lakini Barcelona wanapanga kumnunua tena mchezaji wao huyo wa zamani. Baba wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 alidokeza kuwa Tito Vilanova kuwa meneja wa Barcelona kunafanya mwanae kuwa nafasi kubwa kurejea pale baada ya kuingia matatizoni na kocha wa zamani wa klabu hiyo Pep Guardiola. Klabu yake ya sasa ya Milan inatarajiwa kukutana na Barcelona katika hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Februari mwakani.

No comments:

Post a Comment