Monday, December 10, 2012

FEDERER AKUTANA NA PELE.

MCHEZAJI tenisi nyota duniani Roger Federer amekutana na nguli wa soka wa zamani duniani Pele nchini Brazil mwishoni mwa wiki. Federer alikwenda kumtembelea Pele nyumbani kwake nchini humo na kwenda kubadilishana zawadi na mmoja wa wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya mchezo wa soka. Pele alipewa fulana ya tenisi yenye ujumbe maalumu kutoka kwa Federer wakati naye alimpa nyota huyo wa tenisi fulana yake aliyokuwa akiitumia miaka 1960 ambayo imesainiwa nay eye mwenyewe. Federer alikuwa nchini Brazil kwa ajili ya michuano ya maonyesho ambayo imeandaliwa na kampuni ya Gillette akiwa pamoja na nyota wengine kama Maria Sharapova, Caroline Wozniacki, Serena Williams na Jo-Wilfried Tsonga.

No comments:

Post a Comment