Tuesday, December 4, 2012

MSHIRA KIBENDERA AFARIKI BAADA YA KIPIGO.

MSHIKA kibendera Richard Nieuwenhuizen raia wa Uholanzi amefariki dunia baada ya kupigwa na wachezaji wakati akichezesha mechi ya vijana ambayo mwanae wa kiume naye alikuwa akicheza. Mwamuzi huyo alianguka na kukimbizwa hospitali masaa machache baada ya wachezaji wa klabu ya Nieuw Sloten ya Amsterdam kumshambulia kwa ngumi na mateke katika mchezo huo. Klabu ya Buitenboys ambayo walikuwa wakicheza na Sloten wamesema kuwa mshika kibendera huyo mwenye umri wa miaka 41 alifariki Jumatatu jioni lakini hawakuweka wazi kilichosababisha kifo chake. Mwenyekiti wa Buitenboys, Marcel Oost alionyesha kushangazwa na kilichotokea haswa ukizingatia vijana wenyewe waliokuwa wakicheza walikuwa na umri kati ya miaka 15 na 16. Wachezaji watatu ambao miaka yao ni kati 15 na 16 walikamatwa mapema Jumatatu wakituhumiwa kuwa vinara wa kuanzisha vurugu hiyo ya kumpiga Nieuwenhuizen na kumsababishia umauti.

No comments:

Post a Comment