Sunday, December 23, 2012

STURRIDGE KUFANYIWA VIPIMO VYA AFYA LIVERPOOL.

MSHAMBULIAJI wa Chelsea Daniel Sturridge anatarajiwa kwenye Merseyside baadae leo kwa ajili ya vipimo vya afya ikiwa ni sehemu ya hatua ya kutaka kuhamia katika klabu ya Liverpool. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza anatarajiwa kufanyiwa vipimo katika uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo wa Melwood lakini inaaminika kuwa tayari wameshafikia makubaliano juu ya masuala ya mkataba. Liverpool wanatarajiwa kulipa kiasi cha euro milioni 14 kwa ajili ya mshambuaji huyo mwenye umri wa miaka 23. Klabu hiyo ilikuwa ikihitaji mshambuliaji mapema katika dirisha dogo la usajili Januari mwakani baada ya kucheza nusu ya msimu wakimtegemea mshambuliaji mmoja Luis Suarez.

No comments:

Post a Comment