Monday, January 28, 2013

ABIDAL ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI BAADA YA UCHUNGUZI.

BEKI wa kushoto wa klabu ya Barcelona, Eric Abidal ameruhusiwa kutoka hospitalini baada ya kufanyiwa vipimo kufuatia upasuaji wa kupandikiza moyo aliofanyiwa April mwaka jana. Beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa aligundulika kuwa na uvimbe wa kansa katika ini lake Machi 2011 ambao ulimhitaji kufanyiwa upasuaji mkubwa lakini upasuaji huo haukutatua tatizo hilo moja kwa moja. Mwaka mmoja baadae klabu yake ilitangaza kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 atatakiwa kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza ini jingine na mwezi mmoja baada alifanyiwa upasuaji huo uliokuwa na mafanikio. Abidal anategemewa kujiunga na wenzake mazoezini wiki ijayo baada ya kufanyiwa vipimo kuangalia maendeleo ya ukuaji wa ini lake jipya ambalo alipewa na mpwa wake. Beki huyo hatacheza mchezo wowote wa mashindano toka Februari mwaka jana wakati wa mchezo baina ya Barcelona na Atletico Madrid ambao walishinda kwa mabao 2-1. 

No comments:

Post a Comment