Tuesday, January 29, 2013

USHINDI LAZIMA NA UWEZO TUNAO - RENARD.

KOCHA wa mabingwa watetezi wa michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon Zambia, Herve Renard amesema kuwa ni lazima wapate ushindi katika mchezo wao wa mwisho dhidi ya Burkina Faso utakaochezwa katika Uwanja wa Mbombela baadae leo. Renard amesema wapinzani wao Burkina faso wanahitaji sare yoyote ili wasonge mbele huku wao wakihitaji ushindi wa aina yoyote lakini hilo haliwakatishi tamaa kwani walishakutana na hali kama hiyo katika michuano hiyo mwaka jana. Kocha huyo alitamba kuwa kikosi chake kinaweza kushinda mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa baadae leo na kuweka matumaini ya kutetea taji lao kwa kusonga mbele katika hatua ya robo fainali. Katika mchezo mwingine wa Kundi C Nigeria nao watakuwa na kibarua kigumu wakati watakapocheza na Ethiopia jijini Rustenburg ambapo yoyote atakayepata ushindi kwenye mchezo huo atasonga mbele kwenye hatua ya robo fainali.

No comments:

Post a Comment