Tuesday, January 29, 2013

STARS KUCHUANA NA CAMEROON.

TIMU ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki na Cameroon mchezo ambao utapigwa Jumatano ijayo katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi inatarajiwa kuwa na nyota wote wan chi hiyo akiwemo mshindi mara nne wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Afrika Samuel Eto’o na kiungo wa Barcelona Alex Song ambao wote wamejumuishwa katika kikosi cha wachezaji 21 walioitwa. Mabingwa hao wa zamani wa Afrika wanatarajiwa kukutana jijini Amsterdam kabla ya kuelekea jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo wao na Taifa Stars. Shirikisho a Soka nchini-TFF lipo katika mchakato wa maandalizi ya mchezo huo ambao katika siku chache zijazo kila kitu kitakuwa tayari. Cameroon ilishindwa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika kwa mara ya pili mfululizo baada ya kutolewa na Cape Verde ambao wametinga robo fainali ya michuano hiyo inayoendelea nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment