Monday, January 28, 2013

GALATASARAY YAKIRI KUMNYATIA DROGBA.

KLABU ya Galatasaray ya Uturuki imethibitisha kuwa wako katika mazungumzo ya kuangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji mkongwe wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo ulidai tayari wamwshaanza mazungumzo rasmi juu ya uhamisho wa nyota huyo kutoka klabu ya Shanghai Shenhua ya China. Kuna tetesi zimeripotiwa katika magazeti ya huko yakidai kuwa wamefikia makubaliano na nyota huyo na atapatiwa mkataba wa miezi 18 huku akipewa posho ya euro 30,000 katika kila mchezo ataocheza. Drogba mwenye umri wa miaka 34 aliondoka Chelsea kwenda China mwaka jana baada ya kuisadia Chelsea kunyakuwa taji lake la kwanza la michuano ya Klabu Bingwa ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment