Monday, January 28, 2013

RANI KHEDIRA AONGEZWA MKATABA STUTTGART.

KLABU ya VfB Stuttgart ya nchini Ujerumani imetangaza kumuongeza mkataba utakaofikia tamati 2015 kinda wake Rani Khedira ambaye ni mdogo wa nyota wa kimataifa wa Ujerumani na klabu ya Real Madrid Sami Khedira. Rani ambaye ametimiza miaka 19 Jumapili iliyopita tayari amepandishwa katika kikosi cha kwanza cha Stuttgart ingawa kiungo huyo bado hajacheza mchezo wowote katika Ligi Kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga. Kiungo huyo ambaye yuko katika kikosi cha vijana chini ya miaka 19 cha nchi hiyo amesifiwa na Mkurugenzi wa Michezo wa Stuttgart Fredi Bobic kama mchezaji mwenye kipaji na atakaekuwa na uwezo mkubwa kusakata kabumbu katika siku za usoni. Sami Khedira ambaye ameshacheza michezo 36 ya kimataifa na Ujerumani alicheza katika klabu ya Stuttgart kwa kipindi cha miaka 15 kabla ya nyota huyo mwenye miaka 25 kutimkia Madrid baada ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010.

No comments:

Post a Comment